Pages

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

Monday, April 13, 2015

TANZANIA MPYA YACHANGIA $3000 KWA AJILI YA KUSAIDIA WALIO ZALIWA NA UALBINO

TANZANIA MPYA, kundi la whatsaap la watanzania wanadiaspora lilianzishwa kwa lengo la kuwaunganisha vijana kwa ajili ya kujishirisha katika mijadala ya mawazo ya kuleta chachu ya maendeleo katika jamii ya watanzania marekani na nyumbni Tanzania.

Kundi hili limewahusisha vijana wenye taaluma mbalimbali kwa lengo la kurejea matatizo ya jamii na taifa lao la Tanzania, na kuangalia wajibu na uezo wao katika kushiriki kupigana na changamoto hizo.

Vijana hawa wakidai kuwa wamechoshwa na hulka ya waliowengi, kukaa pembeni na kulaumu serikali.

Akidai Admin wa kundi hili Bwana Nassor Basalama kuwa kazi ya kujenga nchi ni ya wananchi. Sasa ikiwa mwananchi ndio anayefanya kazi ya kulalamika, nani atakaye fanya kazi ya kujenga? Hii ni hulka ya kukosa miono naya kifukara ya kutafuta kujiridhisha kwa kutobeba majukumu mazito ya ujenzi wa taifa.

Kundi hili limewahusisha viongozi wa Jumuiya zote za watanzania marekani, na taasisi mbalimbali.
Wiki 2 zilizopita kundi hili lilikabidhi $3000 kwa NGO ya Albino charity na AFROBINO kwa lengo la kusaidia watanzania wanaoathirika kwa ugonjwa wa ngozi na macho. Pia kundi hili limeandaa powerpoint ambayo imeisambaza kwa jumuiya za watanzania na kwa ajili ya kuelimisha juu ya Albinism. 

CHANZO BLOG YA VIJIMAMBO

0 comments: