Pages

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

Thursday, May 25, 2017

SPIKA WA BUNGE MH. JOB NDUGAI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA RAIS WA KENYA




  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai akisalimiana na Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta wakati wa ibada Maalum ya kuliombea Taifa la Kenya iliyoandaliwa na Bunge la nchi hiyo. Wengine katika  pichani kutoka kushoto ni Spika wa Bunge la Kenya  Justin Muturi, Spika wa Bunge la Seneti la Kenya Mhe  Ekwee Ethuro na Jaji Mkuu wa Kenya Jaji David Maraga. Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la Kenya ambapo amembatana na wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge, Mhe Mary Chatanda, Mhe Salim Turky na Mhe Mch.Peter Msigwa.
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai (katikati ya waliokaa kulia) akizungumza na Rais wa Kenya Mhe Uhuru Kenyatta na Makamu wake Mhe William Rutto walipokutana wakati wa ibada Maalum ya kuliombea Taifa hilo. Wengine katika picha ni Spika wa Bunge la Kenya  Mhe Justin Muturi (kulia kwa Mhe Ndugai),Spika wa Bunge la Seneti la Kenya   Mhe. Ekwee Ethuro  (wa kwanza kulia),Mke wa Rais wa Kenya Margaret Kenyatta na Mke wa Makamu wa Rais wa Kenya Rachel Chebet.
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (wa pili kulia) Mhe Job Ndugai akizungumza na Spika wa Bunge la Seneti la Kenya Mhe Ekwee Ethuro  (wa pili kushoto). Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la Kenya ambapo amembatana na wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge, Mhe Mary Chatanda, Mhe Salim Turky na Mhe Mch.Peter Msigwa.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai akizungumza na Spika wa Bunge la Seneti la Kenya Mhe Ekwee Ethuro  alipomtembelea Ofisini kwake Jijini Nairobi, Kenya. Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la nchi hiyo.

(Picha na Ofisi ya Bunge)


0 comments: