WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirika
la Viwanda vya Sukari nchini Cuba, Bw. Francisco Lled, ambaye amekubali
kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuongeza uzalishaji wa
sukari nchini.
Shirika
la Sukari la nchini Cuba linauwezo wa kuzalisha tani milioni nne za
sukati kwa mwaka huku mahitaji ya ndani ni tani 700,000, ambapo kiasi
kinachobaki huuzwa nje ya nchi. Kwa sasa shirika hilo linazalisha tani
milioni mbili tu katika viwanda vyake 56.
Waziri
Mkuu alikutana na Bw. Lled jana (Alhamisi, Agosti 24, 2017), wakati
alipofanya ziara katika kiwanda cha kuzalisha sukari cha UGB Central
Azucarero 30 de Noviembre katika mji wa San Nicola’s de Bari ambacho ni
kati ya viwanda 27 vya shirika hilo linalomilikiwa na Serikali ya Cuba
kwa asilimia 100.
Katika
mazungumzo yao Waziri Mkuu alimshawishi Bw. Lled kuja nchini kwa ajili
ya kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya kuzalisha sukari. Alisema kwa
sasa Tanzania kuna viwanda vikubwa vitano vya sukari ambavyo uzalishaji
wake hautoshelezi mahitaji ya ndani.
Waziri
Mkuu alivitaja viwanda hivyo ambavyo ni Mtibwa na Kilombero (Morogoro),
Mahonda (Zanzibar), TPC (Kilimanjaro) na Kagera ambavyo vyote
vinazalisha jumla ya tani 320,000 za sukari kwa mwaka huku mahitaji
yakiwa ni zaidi ya tani 400,000.
Hata
hivyo, Waziri Mkuu alisema Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi
inatarajia kujenga viwanda vitatu vya kuzalisha sukari, ambavyo
vitazalisha sukari itakayotosheleza mahitaji na ndani ya nchi na kiasi
kitakachosalia kitauzwa nje.
0 comments:
Post a Comment