NI BAADA YA SHOO YAKE NCHINI NIGERIA
Na Andrew Chale
MBUNIFU mkongwe wa mitindo nchini, Asia Idarous Khamsin kufuatia
kufanya vizuri hivi karibuni katika onyesho kubwa la mavazi ya ubunifu
lililokuwa maalum kwa ajili ya Maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar, lililofanyika Abuja, Nigeria, huku asilimia
kubwa kwenye jukwaa hilo akitumia vazi lililonakshiwa alama za bendela
ya Tanzania, ‘National colours Asia idarous’s design’ tayari watu
mbalimbali duniani wameombwa kutengenezewa mtundo huo.
Akizungumza jiini Dar es Salaam, na mtandao huu, Asia Idarous ambaye pia
ni Mkurugenzi wa Fabak Fashions, alisema kuwa watanzania na raia
mbalimbali wa kigeni duniani kote wametoa order za kutengenezewa vazi
kama hilo ambalo kwa asilimia kubwa limekuwa ni kivutio huku likimweka
mtu yoyote katika hali ya ubora na kupendeza.
Vazi hilo ambalo linabamba ikiwemo aina ya kitambaa maalum na skafu
kubwa inayopachikwa kifuani yenye nakshi ya alam za Taifa, pia tokea
kuwekwa kwenye mitandao ya kijamii na kwenye televisheni nchini Nigeria
na Ulala, imekua gumzo kubwa kwa sasa huku wengine wakishahuri liingizwe
kwenye tukio la kusaka vazi la Taifa.
“Kwa sasa nipo katika kushughulikia oda za wateja wangu ambao wengi
wapo Mataifa ya kigeni ikiwemo Nigeria, Ghana, Kenya, uingereza,
Marekani na kwingineko pamoja na Tanzania” alisema Aisa Idarous.
Alisema kuwa, vazi hilo ambalo pia siku ya onyesho hilo karibu wageni
wote wakiwemo balozi wan chi zaidi ya 61 zilizohudhulia siu hiyo ya
Muungano nchini Nigeria, zilivutiwa na hata kulipongeza kutokana na ua
kielelezo cha Utaifa la Tanzania.
Aidha, Asia Idarous alisema kuwa, matilio ya vazi hilo yapo yanayotoka
nchini Tanzania namengine nje ya nchi ikiwemo Nigeria, tayari baadhi
hoda zimekamilika na baadhi ameanza kuziuza katika duka la Fabak
fashions lililopo Mikocheni mkabara na Kwa Mwalimu Nyerere.
“Hii ni heshima kwangu na kwa Tanzania, kwani vazi hili limeokea
kukubalika duniani kote na kupelekea kuwa utambulisho maalum wa
Mtanzania. Vazi hili kwa kawaida anavaa mtu yoyote na kwenye tukio
lolote lile na hata kumweka mtu katika hali ya umaridadi, ikiwemo kwa
wanaume na wanawake” alisema Asia Idarous.
Asia Idarous pia aliwataka kwa watu watakao taka kuagiza ama kutoa
order, wanaweza kumpigia +255713263363, ama dukani kwake Fabak fashions
Mikocheni kwa Mwl. Nyerere.
0 comments:
Post a Comment