Pages

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

Thursday, May 29, 2014

Rais Jakaya Kikwete Amewasili Toronto Canada kuhudhuria mkutano unaohusu Afya ya Mama na Mtoto kufuatia mualiko kutoka kwa Waziri Mkuu wa Canada Mheshimiwa Stephen Harper.



 Rais Jakaya Kikwete
--
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewasili Toronto Canada tarehe 27 Mei, 2014 usiku  kuhudhuria mkutano unaohusu Afya ya Mama na Mtoto kufuatia mualiko kutoka kwa Waziri Mkuu wa Canada Mheshimiwa Stephen Harper.

Mkutano wa Afya ya Mama na Mtoto , (Maternal, Newborn and Child Health -MNCH) unaanza Leo tarehe 28 – 30 Mei, 2014 ambapo Rais Kikwete pia anatarajiwa kuwa miongoni mwa wazungumzaji wakuu.

Lengo la mkutano huu ni kutoa nafasi kwa wataalamu na viongozi wa dunia kufikia makubaliano kwa pamoja kuhusu jitihada na hatma kuhusu MNCH.

Mkutano huu unatarajiwa kutilia mkazo jitihada za kuimarisha huduma za afya, kuweka kumbukumbu za taarifa, katika jitihada za kupunguza vifo vya mama na watoto wachanga katika nchi zinazoendelea.

Mkutano huu unatarajiwa kuhudhuriwa na kiongozi wa Kidini, Mhe. Aga Khan, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki Moon na Bibi Melinda Gates , ambaye ni Mwenyekiti mwenza wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates.

Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Bi. Margaret Chan na Bw. Antony Lake wa UNICEF.

Akiwa hapa Rais pia atakutana na wadau wa sekta ya biashara na uwekezaji wa Canada na Tanzania kabla ya kurejea Dar es Salaam.


Mwisho

Imetolewa na;
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Toronto-Canada

0 comments: