Bwna Erick Elisha Bahunde picha akiwa hospitali wakati alipopatwa na ajali Photo Via Vijimambo |
Na Abou Sharty Washington DC
Jumuiya
ya waTanzani waishio DMV imeweza kushirikiana katika harambe ya
kumchangia ndugu yetu, Erick Elisha Bahunde ambaye alipatwa na ajali
mbaya wakati alipokuwa akiwajibika kazini na kukatika miguu yake yote
miwili pamoja na mkono wa kushoto, mnamo February 2014. katika Jimbo la
Indiana nchini Marekani.
Harambe
hiyo ulioyongozwa na wana jumuiya wa hapa DMV akiwemu MC Saidi
Mwamende, Katibu wa Jumuiya ya waTanzania , Amos Cherehani, Mchungaji
Malekela Ndugu Faraja Isingo, Mashaka Bilali pamoja na Rais wa Jumuiya
ya waTanzania DMV Bwna Iddi Sandaly.
Watanzania
mbali mbali walihudhuria katika harambe hiyo iliofunguliwa rasmi kwa
dua iliyoombwa na Mchungaji Malekela, na pia kuwaasa watanzania
kushirikiana kwa hali na mali pale mtu yoyote atakaefikwa na misukosuko
yoyote ile ambayo anastahili kusaidiwa asaidiwe.
Mchungaji
Malekela aliendelea kwa kusema kuwa ''Mungu amesema kwamba kama
mwanaadamu anatafuta kuwa na dini safi basi dini safi ndio hii'' kwa
kuweza kujitolea kuwahudumia Wajane, Masikini, Mayatima na wahitaji
wasiyojiweza kama wagonjwa n.k, huku akikumbusha kwamba ''Mungu
ataendelea kugusa watu'' na pia kuwataka waliohudhuria katika ukumbu huo
kuchochea gharama dhidi ya kumchangia mtarajiwa anaestahiki
kuchangiwa.
Baada
ya ufunguzi kwa maneno ya Mungu, waTanzani waliohudhuria katika harambee
hiyo walianza kuchangia michango mbalimbali zikiwemo pesa taslim, cheki
pamoja na vitu ama bidha mbalimbali vilizofikishwa ndani ya ukumbi huo,
pia wale walioahidi kutoa michango na kuandika idadi ya kiwango cha
pesa watakazozitoa walijumuika pamoja na kuaza kutoa michango hiyo, huku
katibu wa jumuiya ya waTanzania DMV Bwna Amos Cherehani pamoja na
Mashaka Bilal wakisherehesha shuhuli hiyo kwa uuzaji wa kunadi bidhaa
hizo zilizofikishwa katika harambee hiyo.
Kulikuwa
na uzwaji wa bidhaa tofauti zilizoletwa na wana waTanzania waishio hapa
DMV zikiwemo vitenge, kanga, gauni, saa za ukutani kopo za kahawa ya
kinyumbani, vitu vyote hivyo viliuzwa na hakuna hata kimoja kilichobakia
katika harambe hiyo na kutimiza kiwango cha $ 4.800 dhidi ya watu
wachache waliohudhuria katika Harambee hiyo ilioandalidwa na Familia ya
Erick Elisha pamoja na Jumuiya ya waTanzania DMV, Siku ya Jumapili June
8, ndani ya ukumbi wa Sligo Creek uliopo Silver Spring Maryland Nchini
Marekani.
Aidhi
Bwna Erick Elisha Bahunde aliwashukuru wale wote waliotoa michango yao
kwa hali na mali kwa kuweza kukamilisha harambee hiyo kwa upendo wao
mkubwa na kujisikia furaha kwa michango hiyo aliyoipa kwa watanzania
wenzake wanaoishi hapa Washington DC.
VIDEO NA PICHA : MUACHE MUNGU AITWE MUNGU NA KAMA HUJAFA HUJAUMBIKA
Mtanzania Elisha Bahunde jina maarufu Eric ambaye siku ya Jumamosi Feb 15, 2014 alipata ajali Jimbo la Indiana iliyopelekea kukatika kwa miguu yote miwili na mkono wa kulia na baadae kuhamishiwa Jimbo la Maryland kwa matibabu zaidi kwa sasa yupo University Of Maryland Medical Center iliyopo 22 S Greene St, Baltimore, MD Ghorofa ya 6 chumba # 8 na anatumia jina la Elisha Bahunde ama kweli hujafa hujaumbika na Mwenyezi Mungu ndiye mueza wa kila jambo ebu sikiliza mwenyewe video hiyo hapo chini na ujionee na picha pia tumekuekea video aliyoshiriki kwenye Kijiwe cha Ughaibuni ameva shati la njano na amekaa karibu na Ally Bambino
Elisha Bahunde akiwa chumba # 8 ghorofa ya 6 alipolazwa tangia siku ya Jumatano Feb 19, 2014 alipoletwa Maryland kwa matibabu zaidi
Elisha Bahunde au Eric akiwa hana miguu wa mkono kama picha inavyoonyesha.
Rais wa Jumuiya DMV, Bwn. Idd Sandaly akiwa Hospitalini hapo kumjulia hali mgojwa
Abdi Makeo amkimjulia hali Elisha Bahunde
Said Mwamende akimjulia hali Bwn. Eric huku akilengwa na machozi
Wanajumuiya waliofika kumjulia hali wakiwa hawaamini walichokiona.
Kutoka kushoto ni Abdi Makeo, Saidi Mwamende, Rais wa DMV Idd Sandaly na Jabir Jongo wakiwa chamba cha mapumziko baada ya kumaliza kumjulia hali Elisha Bahunde kwa jina lingine Eric
Kijiwe No. 44 from Luke Joe on Vimeo.
0 comments:
Post a Comment