Na
Anna Nkinda – Maelezo, New York
Wake wa Marais pamoja na viongozi wametakiwa kuchukua hatua, kutumia sauti zao na nafasi yao ili kuhakikisha watoto, wasichana na wanawake wanapata elimu na afya bora na hivyo kujikwamua na hali ngumu ya maisha.
Wake wa Marais pamoja na viongozi wametakiwa kuchukua hatua, kutumia sauti zao na nafasi yao ili kuhakikisha watoto, wasichana na wanawake wanapata elimu na afya bora na hivyo kujikwamua na hali ngumu ya maisha.
Mwito
huo umetolewa jana na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiongea kwenye
mkutano uliojadili jinsi gani Dunia ichukue hatua kwa ajili ya afya na uchumi
wa wanawake na wasichana uliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Jengo la
Umoja wa Mataifa (UN) mjini New York.
Mama
Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA)
alisema upatikanaji wa elimu bado ni tatizo kwa watoto wa kike hasa katika nchi
zinazoendelea lakini kama watapatikana
watu wa kuwasemea na kuhakikisha watoto hao wanasoma watakuwa
wamewasaidia kuwa na maisha mazuri hapo baadaye.
Alisema
upatikanaji wa huduma za afya na elimu
bora kwa wasichana kutawasaidia
kujikwamua na hali ngumu ya maisha kwakuwa mwanamke ni mlezi wa familia
hivyo basi akiwa na elimu bora hata watoto wake wataweza kusoma na kubadilisha maisha ya jamii zao.
Akizungumzia
kuhusu Taasisi ya WAMA alisema aliamua kuianzisha ili aweze kuwasaidia wanawake
na watoto wa Tanzania hivyo basi wanatoa ufadhili wa masomo kwa watoto wa kike
ambao ni yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi.
“Kwa
upande wa afya tunafanya kazi ya kuimarisha afya ya mama na mtoto kwa kutoa
vifaa tiba katika vituo vya afya, Zahanati na Hospitali, kutoa elimu na
kuhamasisha jamii juu ya upimaji wa
hiari wa ugonjwa wa Ukimwi na saratani za matiti na shingo ya kizazi”.
Pia
tunawawezesha wanawake kiuchumi kwa kuwapa elimu ya ujasiriamali na kuwaongezea
mitaji katika vikundi vyao vya ujasiriamali jambo ambalo limewafanya waweze
kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji mali na kuongeza kipato cha familia”,
alisema Mama Kikwete.
Akiwakaribisha wake wa marais waliohudhuria mkutano huo Mke wa waziri mkuu wa Belize Dean Barrow, Mama Kim Simplis Barrow alisema wake wa marais wananafasi ya kufanya kazi ya kuisaidia jamii yao hasa kina mama na wasichana ambao wameachwa nyuma kimaendeleo ukilinganisha na wanaume.
Mama
Barror alisema ili wake hao wa marais waweze kufanya kazi wanahitaji kupata
rasilimali fedha na watu na kuwataka wadau waliohudhuria mkutano huo
kushirikiana kwa pamoja ili kuhakikisha wanawake wanapata haki zao za msingi
zikiwepo za afya na elimu.
Alisema,
“Wanawake wengi wanapoteza haki yao ya kupiga kura kama tutamia sauti zetu na
kuwaelimisha wataweza kupiga kura,
kupata huduma bora ya afya na hivyo kuweza kuchangia na kushiriki katika
shughuli mbalimbali za maendeleo katika nchi zetu”.
Kwa upande wake Rais wa zamani wa Malawi ambaye alihudhuria mkutano huo kama mwanamke mashuhuri Barani Afrika Joyce Banda aliwataka wake hao wa marais kuwekeza na kuwasaidia wanawake na watoto kwani Mwenyezi Mungu amewapa nafasi hiyo makusudi na wakifanya hivyo matokeo yake yataonekana nanimwanzo wa kupata viongozi wazuri kwa siku zijazo.
Rais Banda alisema karibu Dunia itasherehekea miaka 20 tangu mkutano wa kimataifa wa wanawake ufanyike Beijing nchini China ambao uliweka mwelekeo wa hatua za usawa wa kijinsia na mafanikio yamepatikana kwani kwa sasa wanawake wananguvu na wameweza kushika nafasi mbalimbali za uongozi tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Kwa upande wake Rais wa zamani wa Malawi ambaye alihudhuria mkutano huo kama mwanamke mashuhuri Barani Afrika Joyce Banda aliwataka wake hao wa marais kuwekeza na kuwasaidia wanawake na watoto kwani Mwenyezi Mungu amewapa nafasi hiyo makusudi na wakifanya hivyo matokeo yake yataonekana nanimwanzo wa kupata viongozi wazuri kwa siku zijazo.
Rais Banda alisema karibu Dunia itasherehekea miaka 20 tangu mkutano wa kimataifa wa wanawake ufanyike Beijing nchini China ambao uliweka mwelekeo wa hatua za usawa wa kijinsia na mafanikio yamepatikana kwani kwa sasa wanawake wananguvu na wameweza kushika nafasi mbalimbali za uongozi tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
“Nyie
mnawakilisha watu wengi, fungeni mambo yanayoondoa usawa wa jinsia kwani
matatizo ya wanawake Duniani kote yanafanana. Takwimu zinaonyesha wanawake
wanachangia uchumi wa Duniani kwa asilimia 70 lakini ndiyo waathirika wakubwa
wa umaskini kwakuwa wengi wao wanauchumi
mbovu”.
Wekezeni
zaidi kwa wanawake na wasichana hili liwe ni suala la kitaifa ili wapate elimu ya msingi, sekondari na vyuo kwani
wanaume wanapewa elimu zaidi kuliko wanawake. Wasichana wengi hawaendi shule
kwa ajili ya umaskini lakini wakipata elimu wataepukana na ndoa za utotoni”,
alisema Rais huyo Mstaafu.
Aliendelea
kusema hivi sasa mwanamke akipata ujauzito
hajui kama atapona au atapoteza maisha
hiyo si sawa mwanamke lazima ajifunguea salama na mtoto wake aishi.
Aliwataka kuchukua hatua na kutoa kipaumbele katika kuimarisha afya ya mama
mjamzito na watoto.
Mama
Banda alitumia nafasi hiyo kumpongeza Mama Kikwete kwa kazi anayoifanya ya
kuwasaidia wanawake, wasichana na watoto
wa Tanzania kwa kutatua matatizo yanayowakabili yakiwemo ya afya, elimu na
uchumi.
Mkutano huo ulihudhriwa na wake wa marais kutoka mataifa mbalimbali Duniani, wawakilishi wa mashirika yanayofanya kazi chini ya ofisi za UN, watu na Asasi mbalimbali za Serikali na za kiraia zinazofanya kazi za kuwainua wanawake na kusimamia usawa wa kijinsia uliandaliwa na mke wa waziri mkuu wa Belize Mama Kim Simplis Barrow ambaye ni mwakilishi maalum wa kina mama na watoto na Balozi wa michezo maalum ya Olympics tangu mwaka 2008.
Mkutano huo ulihudhriwa na wake wa marais kutoka mataifa mbalimbali Duniani, wawakilishi wa mashirika yanayofanya kazi chini ya ofisi za UN, watu na Asasi mbalimbali za Serikali na za kiraia zinazofanya kazi za kuwainua wanawake na kusimamia usawa wa kijinsia uliandaliwa na mke wa waziri mkuu wa Belize Mama Kim Simplis Barrow ambaye ni mwakilishi maalum wa kina mama na watoto na Balozi wa michezo maalum ya Olympics tangu mwaka 2008.
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment