Pages

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

Tuesday, August 8, 2017

ROSE MMBAGA ASHINDA TUZO YA MWANAMKE MWENYE USHAWISHI



Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Msichana wa kitanzania, Rose Mmbaga ameweza kushinda tuzo ya Mwanamke mwenye Ushawishi ‘Women in Events Hall of Fame’ ya nchini Marekani na kuwa ni Mwafrika pekee katika kusaidia vijana katika maswala ya masuala ya Mazingira.

Mmbaga ameshinda tuzo hiyo kutokana na uwezo wake wa ushawishi katika kazi za kijamii ambazo amezifanya nchi nzima.

Amesema kuwa Safari yake ilianza na kujitolea kwa takribani miaka mitatu baada ya kuona ajira zinasumbua, na alianza na VSO international kwenye mradi wa International Citizen Service alafu nikajiunga na Restless development katika mradi wa kijana tung’are kazini chini ya International Citizen Service programu kwa takribani miezi sita na tena nikaenda Raleigh Tanzania kwenye mradi wa Expedition.

“nilijenga shule kusaidia watoto yatima,mashirika yote nilishirikiana na vijana kutoka ndani na nje ya nchi na miradi ilifadhiliwa na DFID yani serikali ya wingereza.Haikua rahisi lakini leo hii naweza kuona matunda ya kujitolea katika jamii yangu.”amesema Rose.

Kupitia safari yangu leo hii nimeweza kupata tuzo ya kimataifa kutoka Association for women in events,Hall of fame kama “Woman of Influence”(Mwanamke mwenye ushawishi) ambayo walioniwezesha ni watu ambao wanafahamu kazi yangu na nilioshirikiana nao katika kazi zangu haswa vijana wa kitanzania na wengi wao ni wale waliojitolea

Amesema pongezi zinamwendea mwanaharakati wa kuwasaidia wanawake duniani Mandy Sanghera ameweza kuwa wa kwanza kuninominate jina langu kati ya wanawake wengi na leo hii ninamshukuru kwa kupitia yeye nimeweza kushinda.

0 comments: