Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda na ujumbe wa Tanzania wakilisha samaki katika Bustani Maalum iliyopo katika Malazi ya Viongozi katika Mji wa Kyoto wakati walipofanya ziara ya kutembelea Mji huo leo asubuhi. Mhe. Spika na Ujumbe wa wabunge watano wapo Nchini Japan kwa mwaliko maalum wa Kibunge ikiwa ni sehemu ya kukuza demokrasia ya Nchi hizi Mbili.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akitizama vivutio vilivyopo katika mojawapo ya Madhehebu ya Kijapan (Temple ) wakati walipofanya ziara ya kutembelea Mji huo leo asubuhi. Mhe. Spika na Ujumbe wa wabunge watano wapo Nchini Japan kwa mwaliko maalum wa Kibunge ikiwa ni sehemu ya kukuza demokrasia ya Nchi hizi Mbili. Kushoto kwake ni Mhe. Anne Kilango Malecela
Mhe. Spika akipata maelezo kuhusu utalii na vivutio vilivyopo katika madhehebu hayo wakati wa ziara ya maeneo mbalimbali katika mji wa Kyoto
Mkuu wa dhehebu mojawapo la watu wenye asili ya Japan (Kushoto) (Master of Tenryu – ji Temple) akionesha namna ya kuabudu kwa hisia kwa waumuni wa madhehebu hayo wakati Mhe. Spika na Ujumbe wake walipo tembelea dhehebu hilo kujifunza tamaduni za watu wa Japan. Kutoka kulia ni Mhe. Tundu Lissu, Mhe. Godfrey zambi, Mhe. Anne kilango, Mhe. Anne Makinda (Spika) na Mhe. James Lembeli
Mhe. Spika na Ujumbe wake wakipata maelezo kuhusu dhehebu hilo la Tenryu – ji Temple na jinsi wanavyo abudu
Mkuu wa dhehebu mojawapo la watu wenye asili ya Japan (kulia) (Master of Tenryu – ji Temple ) akionesha vivutio mbalimbali na nakshi zilizomo katika dhehebu hilo wakati ujumbe wa Tanzania ulipofanya ziara kutembelea vivutio mbalimbali katika Mji wa Kyoto. Spika na Ujumbe wa wabunge watano wapo Nchini Japan kwa mwaliko maalum wa Kibunge ikiwa ni sehemu ya kukuza demokrasia ya Nchi hizi Mbili. Picha na Owen Mwandumbya
0 comments:
Post a Comment